HomeRadio Vaticana
foto testata  

Categories


  Charity & Solidarity


  Church


  Culture & Society


  Vatican Documents


  Synod


  Ecumenism


  Family


  Youth


  Justice & Peace


  Politics


  Religion & Dialogue


  Science & Ethics


  Audiences
   & Angelus



  Pastoral visits


cx_t06

CTV - You tube

CTV



 home > Church > news


04/11/2009 9.49.31



Msalaba ni kielelezo cha upendo, umoja na huruma ya Mungu kwa watu wake! Si chanzo cha chuki na uhasama!






Baraza la Maaskofu Katoliki Italia limesikitishwa sana na uamuzi wa Mahakama kuu ya Jumuiya ya Ulaya inayoshughulikia haki msingi za binadamu, kutoa amri ya kuondolewa kwa misalaba yote iliyotundikwa kwenye shule na taasisi za elimu, kama njia ya kuheshimu uhuru wa kidini.

Maaskofu wanasema, huu ni uamuzi ambao unapata chimbuko lake katika masuala ya kisiasa, kiasi cha kusahahu au kushindwa kutambua maana ya Msalaba kwamba si tu kielelezo cha kiimani bali pia unafumbata mwelekeo wa kitamaduni.

Uwepo wa Msalaba katika maeneo ya hadhara ni mang'amuzi na utambuzi wa mchango wa misingi ya kikatoliki na urithi wa wananchi wa Italia, kama inavyobainishwa kwenye Makubaliano ya Mwaka 1984. Maaskofu wanasema, uamuzi huu wa mahakama unataka kutenganisha kimsingi utambulisho wa kitaifa, misingi ya maisha ya kiroho na kitamaduni. Hali hii inaweza kuzua kinzani na migongano isiyokuwa ya lazima.

Padre Federico Lombardi, Msemaji mkuu wa Vatican anabainisha kwamba, kimsingi Msalaba ni kielelezo cha upendo wa Mungu, umoja na mshikamano kati ya watu. Inasikitisha kusikia kwamba, Msalaba sasa unakuwa ni kielelezo cha kinzani, migawanyiko na ukosefu wa uhuru. Mawazo kama haya ni kinyume kabisa na uelewa wa wananchi wa Italia.

Ni jambo lisilokubalika kuondoa katika mazingira ya elimu, kielelezo cha tunu msingi za kidini, katika historia na utamaduni wa watu wa Italia. Dini inachangia kwa kiasi kikubwa katika majiundo na makuzi ya mwanadamu kimaadili, na kielelezo makini cha utamaduni na maendeleo ya mtu. Ni kosa la kiufundi na mwono finyu kabisa kung'oa Msalaba katika maeneo ya majiundo ya watu.

Padre Federico Lombardi anasema, kitendo hiki kinasikitisha na kutia uchungu, kwani mwelekeo wa sasa ni kutotaka kutambua mchango wa Kikristo katika majiundo ya watu wa Ulaya, ukweli ambao kamwe hautaweza kupindishwa.


  « back to index

 






04/11/2009 11.03.01
Benedikto XVI kuongoza Ibada ya kuwaombea marehemu Makardinali na Maaskofu Siku ya Alhamisi asubuhi


04/11/2009 10.11.37
Taarifa ya ziara ya mkaguzi wa kitume kwa mashirika ya kitawa nchini Marekani: matumaini na wasi wasi kwa siku za usoni!


03/11/2009 11.47.24
"Wasindikizeni mapadre wenu kwa sala na sadaka katika hija yao ya utakatifu wa maisha"


03/11/2009 11.22.39
Lake Victoria - the next international symposium on Religion, Science and Environment.


03/11/2009 11.07.14
The work and the Message of the Synod: Pope Benedict reflects.




Related categories


Page précédente  Previous page
Page d'accueil  Home Page
Ecrire à la rédaction  Contact us
top
top
All the contents on this site are copyrighted ©. Webmaster / Credits / Legal Conditions
top
top