HomeRadio Vaticana
foto testata  

Categories


  Charity & Solidarity


  Church


  Culture & Society


  Vatican Documents


  Synod


  Ecumenism


  Family


  Youth


  Justice & Peace


  Politics


  Religion & Dialogue


  Science & Ethics


  Audiences
   & Angelus



  Pastoral visits


cx_t16

CTV - You tube

CTV



 home > Audiences & Angelus > news


04/11/2009 10.52.52



Taalilimungu ya moyo ikuze majadiliano na taalilimungu akili, ili kuondokana na kiburi cha kisomi katika mafumbo ya imani






Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, siku ya jumatano, tarehe 4 Oktoba, 2009 aliendelea na katekesi yake, akifanya ulinganisho wa kitaalimungu kati ya Mtakatifu Bernard Clairvaux na Mtakatifu Abelard, wote ni wasomi wanaongaliwa katika mwelekeo wa imani inayotafuta kufahamu zaidi. Baba Mtakatifu anasema, mahali ambapo Mtakatifu Bernard alipenda kukazia zaidi kuhusu imani, Mtakatifu Abelard akaweka msisitizo kwenye uelewa.

Taalimungu mintarafu Mtakatifu Bernard ilipania kumwezesha mwamini kuwa na mang'amuzi ya Mungu dhidi ya kiburi cha kisomi, kinachowafanya baadhi ya watu kudhani kwamba, wanaweza kuyafahamu mambo yote yanayojikita katika Fumbo la Imani.

Mtakatifu Abelard alipania zaidi kutumia mang'amuzi ya kifalsafa katika taalimungu na hatimaye, kung'amua kutoka katika dini za watu wengine ile mbegu inayowafunulia uelewa wa Kristo. Maelekeo haya mawili anasema Baba Mtakatifu kati ya watakatifu Bernard na Abelard; taalimungu ya moyo na taalimungu ya akili yalizua kinzani.

Yote haya yanabainisha umuhimu wa majadiliano ya kina katika medani ya kitaalimungu na utii kwa viongozi wa Kanisa. Taalimungu haina budi kuheshimu misingi iliyopokelewa kutoka katika Ufunuo inapoendelea kuipatia tafsiri sahihi kadiri ya mwanga wa kifalsafa.

Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita anasema, kunapotokea kinzani za kitaalimungu, kila mtu, lakini kwa namna ya pekee, viongozi wa Kanisa wanao wajibu wa kulinda na kuhifadhi imani katika ukamilifu wake. Baba Mtakatifu anawaombea waamini wanapoendelea kujifunza Injili, Mwenyezi Mungu aweze kuwaimarisha katika ukweli na upendo.

Baba Mtakatifu akizungumza na waamini pamoja na mahujaji kwa lugha mbali mbali amewaasa kuwa waaminifu kwa imani iliyofunuliwa kwa Mama Kanisa pamoja na kujitahidi kuwa ni wahudumu wa ukweli na upendo kwa moyo na akili zote.

Baba Mtakatifu akizungumza na waamini kutoka Poland alimkumbuka Mtakatifu Karoli Borromeo, ambaye Mama Kanisa anafanya kumbu kumbu yake tarehe 4 Novemba, kila mwaka kwa kuelekeza mawazo yake kwa Hayati Baba Mtakatifu Yohane Paulo wa pili.

Mfano wa maisha na mafundisho yake yawaimarishe waamini katika imani pamoja na kuwapatia changamoto ya kuchuchumilia utakatifu wa maisha. Amekazia pia moyo wa sala unaojikita katika nyimbo za kidini, kama njia ya kushehenesha mioyo kwa imani na matumaini, ili hatimaye, kutolea ushuhuda wa imani, kwa kutangaza matendo makuu ya Mungu katika maisha.



  « back to index

 






16/11/2009 8.27.37
Waamini wamesindikizwa katika hija yao ya kiroho hapa duniani kipindi cha Mwaka wa Kanisa kwa tafakari ya Injili ya Marko


11/11/2009 15.31.42
Papa aihimiza serikali ya Sri Lanka kuharakisha juhudi za wakuwarudisha wakimbizi makwao


02/11/2009 9.19.01
Kumbukumbu ya miaka 10 ya kutiwa sahihi hati ya kuhesabiwa haki, izidishe ari na mwamko wa majadiliano ya kiekumene na ushuhuda wa pamoja


02/11/2009 8.53.26
Benedikto XVI anawaalika waamini kuwakumbuka mapadre wao watakatifu waliowawezesha kukua katika imani


28/10/2009 15.26.20
Mshikamano wa Imani na hoja ni mabawa mawili ya binadamu- Papa



Related categories


Page précédente  Previous page
Page d'accueil  Home Page
Ecrire à la rédaction  Contact us
top
top
All the contents on this site are copyrighted ©. Webmaster / Credits / Legal Conditions
top
top