HomeRadio Vaticana
foto testata  

Categories


  Charity & Solidarity


  Church


  Culture & Society


  Vatican Documents


  Synod


  Ecumenism


  Family


  Youth


  Justice & Peace


  Politics


  Religion & Dialogue


  Science & Ethics


  Audiences
   & Angelus



  Pastoral visits


cx_t12

CTV - You tube

CTV



 home > Justice & Peace > news


05/11/2009 8.58.34



Mshikamano wa dhati, mafao ya kizazi kijacho na mabadiliko ya mtindo wa maisha; ni mambo ya kuzingatiwa katika agenda ya nishati






Askofu mkuu Celestino Migliore, Mwakilishi wa Kudumu wa Vatican kwenye Umoja wa Mataifa anasema, teknolojia rafiki inayoheshimu na kutunza mazingira, mapambano dhidi ya umaskini, ushirikiano wa kimataifa unaojengeka katika misingi na kanuni ya auni, ubadilishanaji wa taarifa na teknolojia ni kati ya mambo ambayo yanaweza kusaidia Jumuiya ya Kimataifa kulinda na kutunza mazingira.

Askofu mkuu Migliore anasema, Nchi Changa duniani zinauwezo wa kudhibiti uchafuzi wa mazingira ikiwa kama zitawezeshwa kwa njia ya mtaji na teknolojia, ili kutumia umeme wa jua na ule unaozalishwa kutokana na maporomoko ya maji, bila kusahau uwezekano wa kuwa na matumizi ya nishati uoto. Mwelekeo huu utaziwezesha nchi changa duniani kukabiliana kwa kiasi kikubwa na ongezeko la mahitaji ya nishati pamoja na kujiletea maendeleo endelevu.

Majadiliano kuhusu nishati hayana budi pia kuangalia madhara yanayoweza kuwapata binadamu na uharibifu wa mazingira kwa siku za baadaye. Busara na umakini katika maamuzi ya kimataifa kwani madhara ya uchafuzi wa mazingira ni matokeo ya nchi zilizoendelea duniani, lakini nchi maskini zinaathirika pia kutokana na maamuzi haya bila kusahahu changamoto za mabadiliko ya tabianchi.

Askofu mkuu Celestino Migliore anasema, matumizi ya teknolojia rafiki ni changamoto kuanzia kwa mtu binafsi, sekta binafsi na serikali katika ujumla wake. Matumizi ya nishati yazingatie pia haki kwani, kizazi kijacho kinaweza kuonja pia madhara ya matumizi tenge ya nishati duniani, hali ambayo inahitaji Jumuiya ya Kimataifa kubadili mtindo wa maisha yake, kwa kukazia kanuni ya mshikamano unaovuka mipaka ya kitaifa na kiuchumi.

Matumizi ya nishati inapaswa kuwa pia ni agenda katika masuala ya kielimu, ili kuwawezesha wananchii kuwa na sera nzuri katika maendeleo ya nishati na matumizi yake kama njia ya kudhibiti mabadiliko ya tabianchi na madhara yake katika jamii.


  « back to index

 






07/11/2009 10.54.39
Imani thabiti ilichangia kuanguka kwa ukuta wa Berlini, miaka ishirini iliyopita!


05/11/2009 9.23.15
Mji wa Yerusalem hauna budi kuwa ni kitovu cha amani na suluhu ya migogoro katika Nchi Takatifu


04/11/2009 13.06.37
Sheria ya watoto Tanzania kuhakikishia haki zao msingi


03/11/2009 8.29.27
Wakimbizi kutoka Burundi waanza kurudi nchi mwao, wanahitaji moyo wa uvumilivu na upendo ili kuijenga nchi yao kwa pamoja


31/10/2009 11.26.27
GMOs ? Who would they really help ?



Related categories


Page précédente  Previous page
Page d'accueil  Home Page
Ecrire à la rédaction  Contact us
top
top
All the contents on this site are copyrighted ©. Webmaster / Credits / Legal Conditions
top
top